Kama unataka kuuza Virutubisho Lishe Bila Kuchat na wagonjwa…

Igilizia Na UKopi Mfumo Huu Mpya Wa Kuuza Virutubisho Lishe Kutoka Kwa Vincent James Ambae Aliwahi Kutumia Mfumo Huu Kuuza Virutubisho Lishe Na Kutengeneza Faida ya Dola Za Marekani Milion 100 Ndani Ya Miezi 23 Tu.

Mfumo Huu Unafanya Kazi Kwa Niaba Yako Masaa 24 Na Wala Huhitaji Kuwa Na Group Lolote Whatsapp Au Kuchat Na Mgonjwa Yeyote Inbox. Kwa Kutumia Mfumo Huu Utafanya Kazi Dakika 30 Tu Kila Siku!

Kutoka kwa: Mr Bokko

Social media Marketing & Advertising Expert.

Dar Es Salaam.


Mpendwa Networker,

Kama unatumia magroup ya whatsApp, WhatsApp Inbox, messenger au Instagram inbox kuuza virutubisho lishe vyako kuna hela nyingi sana unaziacha mezani.

Kabla sijakwambia kivipi naomba nikuulize swali:

Unaweza kuchat na wagonjwa wapya 200 kila siku bila kuhisi kuzidiwa?

Jibu ni hapana.

Unaweza kuwa na magroup whatsapp zaidi ya 20 ambayo yote kila siku yanakuhitaji upost kitu kipya bila kuhisi kuzidiwa?

Jibu ni hapana.

Ndio maana nimekwambia kuna hela nyingi unaziacha mezani kama unauza virutubisho lishe vyako kwa kuchat na watu whatsapp, messenger au instagram inbox.

Kwasababu pindi unapoacha kuchat na mtu mpya au kupost kwenye group hutengenezi hela yoyote.

Fikiria wakati unafanya mazungumzo na rafiki zako, ndugu zako au unafanya shughuli zingine maana yake hakuna kuuza kwasababu kuuza kwako ni mpaka uchat na mtu mpya au upost kitu kwenye magroup yako.

Kama ilivyokuwa kwangu, nina imani hata wewe ulijiunga kwenye network marketing ili upate uhuru wa Muda na wa kipato.

Sasa…

Unahisi kwa kutumia whatsapp, messenger, instagram inbox utapata uhuru wa muda au kipato?

Jibu ni hapana.

Kwasababu ili utengeneze pesa itakubidi muda mwingi (Kama sio wote) uwe umeganda kwenye simu yako unachat na wagonjwa. Au…

Upo bize unaandaa maudhui (Content) ya kupost kwenye magroup yako.

Ni kweli kwa kutumia platform hizo utapata wagonjwa wa kununua virutubisho lishe vyako lakini kwa kufanya kazi sana kama punda na…

Si hivyo tu…

Utatengeneza hela kidogo wakati hela nyingi utaziacha mezani. Unajua kwanini?

Zipo sababu 2 kwanini unaacha hela mezani kwa kutumia platform hizo. Ngoja nikuelezee:

Sababu ya kwanza: Unafanya kazi ndani ya biashara yako badala ya kufanya kazi kwenye biashara yako!

Kazi ya gari ni kukutoa wewe sehemu moja kwenda nyingine kwa haraka zaidi. Sasa wewe badala ya kulipanda gari likupeleke unakotaka kwenda unalisukuma. Unahisi kwa kulisukuma utafika lini unakoenda? Itakuchukuwa muda mrefu kufika unakoelekea na mpaka unafika utakuwa umechoka sanaaaaaaaa. Kwahiyo…

Kufanya kazi ndani ya biashara yako ni sawa na kulisukuma gari  maana yake wewe mwenyewe ndo unatumika kama kila kitu kuiendesha biashara yako.

Usipokuwepo au usipofanya chochote biashara yako inasimama

Kumbuka kuna masaa 24 tu kila siku. Hayaongezeki wala hayapungui.

Na wewe utabakia kuwa mmoja.

Na kuna mengi ya kufanya kila siku ukiachana na kuendesha biashara yako.

Kwahiyo kama biashara yako ili iingize pesa inakutegemea wewe 100% maana yake kutokuwepo kwako au kusimama kwako kufanya shughuli za kibiashara ndo habari ya kutengeneza hela inakuwa imeishia hapo.

Kwahiyo muda huo ambao utakuwa hufanyi shughuli za kibiashara kuna hela nyingi sana utakuwa unaziacha mezani zinachukuliwa na wengine.

Na wakati Kwa upande mwingine, kufanya kazi kwenye biashara yako maana yake biashara yako inaendeshwa na mfumo wakati wewe kazi yako ni kuuendesha huo mfumo. 

Kwakua biashara yako inaendeshwa na mfumo maana yake kutokuwepo kwako (Kutochat na wagonjwa inbox au kutopost kwenye magroup) hakuathiri kipato unachokiingiza kwenye biashara yako…

Na unakuwa umeondoa ukuta wa kukuzuia kutengeneza hela nyingi maana licha ya wingi wa wagonjwa mfumo utaweza kuwamudu wote kwa pamoja hata kama wapo 5000.

Sababu ya pili: Kuuza Virutubisho Lishe unahitaji uwanja tulivu na mpana ili kuweza kuitetea bei yako!

Bei ya virutubisho lishe imechangamka sana, yaani ipo juu.

Sasa ni ngumu kumuuzia mgonjwa kwa kuchat nae dakika kadhaa halafu umwambie dozi ya tatizo lake gharama nzima ni 1,000,000/= 

Mgonjwa anaweza kupata mshituko wa moyo wa ghafla kisa bei kuwa kubwa.

Licha ya hivyo…

Wakati unachat nae huenda muda huo huo akawa anachat na watu wengine au wakati anasubiri ujibu meseji yake yupo status anaangalia yaliyojiri. Kiufupi umakini wote wa mgonjwa haupo kwako peke yako. Umegawanyika.

Kwasababu ya kukosa umakini wote wa mgonjwa utakachokisema hakitakuwa na mashiko kwa mgonjwa huyo kununua virutubisho lishe vyako.

Fikiria hospitalini, anakuwa ni mgonjwa mmoja na daktari. Hivyo umakini wote wa mgonjwa unakuwepo kwa anachokisema daktari.

Lakini wewe kwenye group lako whatsapp au inbox mtu huyu wakati huo huo anakuwa na mambo 100 mengine yakiendelea.

Kukosekana kwa umakini wa mtu huyu ukifika wakati wa kumtajia bei kuna uwezekano usimsikie tena kwasababu atakumbuka bei na sio ambacho virutubisho lishe vyako vinaenda kumsaidia na yote ni kwasababu wakati unazungumza nae alikuwa anaendelea na mambo yake mengine.

Ndio maana nimekwambia unahitaji uwanja tulivu ambapo itamlazimu mgonjwa aachane na mambo yake mengine yote akusikilize wewe kwanza utoe maelezo ya kutosha kuitetea bei yako ili ukifika wakati wa kumtajia bei aone ni ya kawaida ukilinganisha na kile ambacho virutubisho lishe vyako vinaenda kumfanyia.

Tazama…

Mpaka 2021 mwezi wa 11 nilikuwa sijawahi kuuza virutubisho lishe na kutengeneza faida ya zaidi ya 600,000/= ndani ya mwezi mmoja.

Na sababu ni kwamba kabla ya 2021 mwezi wa 11 nilikuwa natumia whatsapp kufanya mauzo.

Sio kwamba nilikuwa napenda kutumia whatsApp…

Hapana. Nilikuwa nimeichoka mpaka staki kuisikia.

Kwanza nilianza kwa kuacha kufungua magroup mapya maana hata niliyokuwa nayo ilikuwa imefikia hatua yamenishinda kuyaendesha kila siku. 

Hali ya kutengeneza maudhui mapya ya kupost kila siku ikawa imefika hatua naona ni mateso kwangu.

Licha ya hivyo wagonjwa wengine kwenye group walikuwa hata sio wanunuaji zaidi ya kunichora tu.

Unakuta mgonjwa mmoja yupo kwenye magroup ya watu wengine kama 10 anaangalia sehemu ambayo kuna bei ya chini ndio anunue.

Nikaamua nifute magroup yote na kuapa sitafungua group lolote tena kwa ajili ya kuuza virutibisho lishe.

Nikaanza kuuza kupitia whatsapp inbox.

Mwanzoni nikaona afadhali ya magroup lakini shida ilikuja nilipoanza kurusha matangazo ya kulipia Facebook na Instagram.

Watu wakawa wanakuja wengi mno kama mvua kana kwamba nisingeweza kuwamudu wote kwa wakati huo.

Ikawa inanibidi nizime kwanza matangazo.

Wagonjwa wengine wakawa wanalalamika kwamba nachelewa kujibu meseji zao.

Nilikuwa najikuta kutwa nzima niko bize nachat na wagonjwa halafu unashangaa siku nzima sijauza kwa mgonjwa hata mmoja au nimeuza kwa mgonjwa mmoja tu licha ya kuchat na wagonjwa zaidi ya 200.

Ilifika hatua nikawa nazima kwanza data kwenye simu yangu nitoke whatsapp maana unashangaa ndani ya dakika 5 ushatafutwa na watu zaidi ya 80.

Hali hii ilinifanya niwe mtumwa wa simu yangu maana muda wote lazima ungenikuta nachat tu na wagonjwa.

Kama nilivyokwambia nilikuwa nimechoka kutumia whatsapp kufanya mauzo maana nilikuwa nachoka sanaaaa kila siku halafu mauzo kidogo na kibaya zaidi nikawa sipati muda wa kufanya mambo mengine.

Kwasababu ya kuichoka whatsapp, 2020 mwezi wa 6 ivi nikawa nimegundua mfumo ambao unaweza ukanisaidia kuuza virutubisho lishe vyangu pasipo kuhitaji uwepo wangu.

Nilipougundua mfumo huo nilikuwa na shauku kubwa sanaa ya kuanza kufurahia kuuza virutubisho lishe vyangu pasipo kutumia nguvu nyingi.

Tatizo ni kwamba mfumo huo ulihitaji pesa nyingi kidogo kuutengeneza ili uanze kufanya kazi.

Ikumbukwe 2020 ulikuwa ni mwaka wa korona.

Kwahiyo nikamhusisha rafiki yangu kuhusu mfumo huu na kumuomba ushauri ni kwa jinsi gani tupate pesa ya kutengeneza mfumo huo na pia tubaki na pesa za kutusogeza kwa siku kadhaa.

Rafiki yangu akaona kwa kutumia mfumo huo tutapiga pesa nyingi kwahiyo akaniambia ngoja afanye namna apige simu nyumbani kwao (Mwanza)  aone kama atapata sapoti yoyote ya kifedha. 

Mama yake rafiki yangu akauza akiba yake ya magunia ya mpunga akamtumia rafiki yangu 200,000/=

Na mimi nikaamua nipige simu nyumbani (Kigoma) kuomba sapoti ya kifedha. Dada yangu na shangazi yangu wakajichanga wakanitumia 100,000/=

Kwahiyo tukaongezea hiyo 300,000/= na pesa tuliyokuwa nayo kuweza kutengeneza huo mfumo wa kuuza virutubisho lishe pasipo uwepo wangu.

Mfumo ukatengenezwa. Ikafika muda wa kuujaribu mfumo kuona matokeo yake.

Kuifupisha Stori Ni Kwamba Baada Ya Wiki Moja Za Majaribio, Mfumo Ulitutia Hasara Mpaka Pesa Za Matumizi Tulizokuwa Nazo Zote Ziliisha!

Mfumo uligeuka kuwa zombi ambalo linanyonya kila akiba ya pesa tuliyokuwa nayo (mimi na rafiki yangu)

Baada ya mfumo huo kututia hasara nakumbuka kama vile ilikuwa jana, wiki nzima akili yangu ilikuwa kama vile imeganda. Nilihisi kudata. Nilikuwa mnyonge sanaaaaaaa.

Ndani ya wiki hiyo ya majonzi sikutaka kusikia chochote kuhusu kuuza. Nilikuwa na maumivu makali mno.

Wiki nzima nilikuwa nashinda ndani nimelala naugulia maumivu ya kupoteza hela kwenye mfumo ambao niliamini kwa asilimia zote lazima ufanye kazi.

Hilo likapita. Nikaendelea zangu kuuza kwa kutumia whatsapp (Inbox) lakini kishingo upande.

Mwaka mmoja mbele (2021 mwezi  wa 10 ivi) kwenye pita pita zangu mtandaoni nikakutana na habari za jamaa mmoja wa marekani.

Jamaa huyu anaitwa Vincent James.

Huyu Jamaa Amewahi Kuvunja Rekodi Kwa Kuuza Virutubisho Lishe Na Kutengeneza Faida Ya Dola Za Marekani Milioni 100 Ndani Ya Miezi 23 Tu.

Hiyo dola milioni 100 za marekani kwa pesa yetu ya kitanzania ni sawa na Bilioni 200 na milioni 400 ivi.

Fikiria mtu anatengeneza pesa yote hiyo ndani ya miezi 23 tu.

Kilichonishangaza ni kwamba hakuwa Networker ila aliuza virutubisho lishe.

Na alikuwa anapata wateja wapya elfu arobaini (40000) kila mwezi.

Habari kuhusu huyu jamaa zilinivutia zaidi nikaanza kuchimba na kudadisi ni njia ipi anaitumia huyu jamaa.

Nilijuwa siwezi nikatengeneza kama hela alizozitengeneza lakini kama nikitumia njia aliyoitumia kuna uwezekano mkubwa na mimi nikaanza kutengeneza milioni kadhaa kila mwezi.

Nilivyomfuatilia huyu jamaa kiundani zaidi niligundua kwamba alikuwa na mfumo ambao hauhitaji uwepo wake kutengeneza hela.

Marekani ni tofauti na Tanzania.

Marekani unaruhusiwa kuanzisha kampuni yako mwenyewe ya virutubisho lishe na ikaanza kufanya kazi ndani ya siku au wiki kadhaa tofauti na bongo yetu.

Kwahiyo huyu jamaa alichokifanya aligundua kuna soko na uhitaji mkubwa sana wa virutubisho lishe ndio maana zinafunguliwa kampuni nyingi za network marketing kila iitwayo leo.

Badala ya kujiunga kwenye network marketing…

Alichokifanya alienda kwa wataalamu wa lishe wamchanganyie virutubisho lishe na kutengeneza dawa ambayo ataipa jina la brand yake na kuanza kuiuza kama yake.

Kwakua alikuwa na mfumo mathubuti akaanza kuuza virutubisho lishe hivyo chini ya brand yake na kwa kutumia mfumo wake akawa anapata wateja wapya 40000 kila mwezi.

Ndani ya miezi 23 akawa tayari kavunja rekodi ya kutengeneza milioni 100 za marekani.

Hiyo pesa ni nyingi, nyingi mnooooooo. Sio rahisi kuitengeneza ndani ya muda mfupi hivo. Lakini yeye kwa mfumo wake aliweza.

Nikajifunza kila kitu kuhusu mfumo wake lakini nikagundua kwa Tanzania yetu ni ngumu kuutumia kama ulivyo.

Lazima kuwepo na marekebisho ya kuufanya mfumo uendane na Tanzania yetu.

Si hivyo tu…

Niligundua kwamba mfumo wake umebebwa na ujuzi mmoja unaoitwa “Copywriting” (Nitakwambia maana yake hapo mbele kidogo)

Basi nikaanza harakati za kujifunza ujuzi huo na  kuumiza kichwa ni kwa jinsi gani nifanye marekebisho kwenye mfumo wake ili ufanye kazi kwa Tanzania yetu.

Baada ya majaribio ya wiki kadhaa nikafanikiwa kutengeneza mfumo unaoendana na mfumo wa Vincent James lakini ambao unafanya kazi kwa Tanzania yetu.

Na taarifa njema ni kwamba utengenezaji wa mfumo huu hauhitaji hata senti 5 kama nilivyopoteza pesa nyingine kutengeneza mfumo ambao uliishia kunitia hasara.

Mfumo huu kuutengeneza ni bure kabisa. Hauhitaji vifaa vyovyote vya kulipia.

Kwahiyo nikawa nimeanza kuutumia mfumo huo. Na haya ni baadhi ya matokeo yangu:

Kuanzia hapo nikasema kwaheri ya kuonana whatsapp.

Sijawahi kutumia tena messenger au whatsapp au instagram inbox kama njia ya kupata mauzo.

Sasa nina uhuru wa kufanya mambo yangu mengine bila kuhofia kupata wateja maana mfumo hauhitaji uwepo wangu ndio nitengeneze kipato.

Mara ya mwisho nilitumia mbinu (ambayo nitakufundisha) kuangalia matangazo yote ya kulipia ambayo watu wanayarusha Facebook na Instagram.

Niligundua kwamba 99% ya matangazo yote yanawatoa watu Facebook au instagram kuwapeleka messenger, instagram inbox au whatsapp.

Kwahiyo 99% ya networkers wote wanaofanya matangazo ya kulipia wanaacha pesa nyingi mezani.

Sasa fikiria wewe ukianza kutumia mfumo huu ambao naenda kukuelekeza unadhani nini kitatokea?

Utafagia wateja maana pesa zote zinazoachwa mezani zitakuwa zako.

Na bado huo sio uzuri wa mfumo huu.

Uzuri mkubwa wa mfumo huu ni kwamba kwa kufanya kazi dakika 30 tu kila siku (asubuhi, mchana au jioni kulingana na mapendeleo yako) utaweza kutengeneza faida kubwa wakati ukiendelea kufanya shughuli zako zingine na pasipo kufanya kazi sana kama punda.

Tazama…. kwenye kampuni uliyopo kila mtu anauza bidhaa kama unayoiuza wewe. Na bado kuna makampuni mengine ya network marketing ambayo wanachama wake wananauza bidhaa kama yako.

Kwahiyo kuna ushindani mkubwa sanaaaaa.

Hata hivyo, ushindani ni ishara ya kwamba kuna pesa na watu wananunua.

Lakini unajua njia ambayo kila mmoja wao anaitumia kuuza ni ipi?

Whatsapp, Messenger na Instagram inbox.

Kwahiyo wewe ukitumia mfumo ambao naenda kukuelekeza maana yake utakuwa miongoni mwa watu wachache sana ambao:

  1. Wanatumia nguvu kidogo kutengeneza faida kubwa

  2. Wamejitoa kwenye ushindani

  3. Mfumo unawafanyia kazi ya kuuza virutubisho lishe wakati wao wanaendelea na mambo yao mengine

  4. Hawaachi pesa mezani kwa maana mfumo unafanya kazi masaa 24 kwa niaba yako.

Kwahiyo kama utahitaji nikuongoze kutengeneza mfumo wa namna hii, nitakuwa tayari kukusaidia kwasababu nimeandaa program ambayo inaitwa…

Customer Acquisition Engine (CAE)!

Customer Acquisition Engine

Program hii ni ya wiki 4 (Lakini unaweza kuimaliza kabla ya wiki 4 kuisha kulingana na uelewa wako)

Mpaka wiki 4 (au chini ya hapo kulingana na uelewa wako) kuisha utakuwa tayari umesimamisha mfumo ambao unafanya kazi masaa 24 kukuvutia wateja wakati wewe umelala au unafanya shughuli zako zingine.

Ukiangalia hapo kwenye picha juu utaona mfumo huu umeundwa kwa hatua kuu 2.

Hatua ya kwanza: Before click experience na

Hatua ya pili: After click experience.

Ngoja nikuelezee hatua moja baada ya nyingine.

Hatua ya kwanza: Before click experience

Haya ni jumla ya mambo yote ambayo yanafanyika kwenye mitandaoni ya kijamii (mfano: Facebook au Instagram)

Au kwa maelezo rahisi ni kwamba “before click experience” ni kwenda kwenye mitandao ya kijamii kama Facebook au Instagram kutangaza kwa lengo la kutafuta wagonjwa wenye uhitaji wa virutubisho lishe vyako.

Mgonjwa ambaye atakuwa na uhitaji itambidi akutafute kwa maelezo zaidi.

Kwahiyo hatua zote utakazozifuata kuanzia hatua ya kwanza ya kurusha tangazo lako mpaka hatua ya mwisho ya mgonjwa kuanza kusoma tangazo lako na kubonyeza link kwenye tangazo lako hiyo ndio tunaiita “Before click experience”

Naomba nieleweke vizuri.

Lengo la hatua hii sio kuuza bali kutafuta wagonjwa wenye uhitaji wa virutubisho lishe vyako.

Na wakati…

Hatua ya pili: After click experience.

Haya ni mambo yote ambayo yanatokea (Nje ya mitandao ya kijamii) baada ya mgonjwa kubonyeza link kwenye tangazo lako Facebook au Instagram.

Kwa maelezo rahisi ni kwamba mtu huyu aliyebonyeza kwenye link ya tangazo lako maana yake ana uhitaji wa virutubisho lishe vyako, kwahiyo kinachotokea kwenye hatua hii ya pili kiufupi ni kufanya mauzo.

Hatua ya kwanza ni kutangaza kutafuta mwenye uhitaji wakati hatua ya pili nikumuuzia virutubisho lishe vyako mtu huyu mwenye uhitaji.

Hatua hii ya pili ni mchakato mrefu kidogo.

Kwasababu kama unavyoona kwenye picha hapo juu, baada ya mtu kubonyeza link kwenye tangazo lako atakutana na ukurasa maalumu unaoitwa “sales page

Kazi ya sales page ni kuuza bidhaa yako masaa 24 pasipo uwepo wako.

Mfano wa sales page ni kama ukurasa ambao unausoma muda huu.

Kwahiyo kwa kusoma maneno yaliyopo kwenye sales page yako (Nitakufundisha hatua kwa hatua jinsi ya kuitengeneza) mgonjwa ataweza kuwa tayari kutoa pesa yake na kukupatia wewe umuuzie virutubisho lishe vyako.

Mgonjwa anavyokuwa tayari kutoa pesa atabonyeza link iliyopo mwishoni mwa sales page yako.

Link hiyo itampeleka kwenye ukurasa mpya ambao utakuwa na fomu ya yeye kutuma ODA yake.

Mgonjwa atatuma ODA yake ya DOZI atakayochukuwa na ni muda gani uweze kumtumia na mahali anapoishi.

Baada ya mgonjwa kutuma ODA yake wewe utapata ujumbe kwenye email yako ukikujulisha kwamba kuna mgonjwa kaweka ODA.

Baada ya hapo wewe kazi yako ni moja tu ambayo itakuwa ni kupiga simu na kuongea na mgonjwa ambaye tayari kaweka ODA yake kufanya utaratibu wa kumtumia Bidhaa.

Hapo nimekuelezea mfumo huu kiufupi.

Kama nilivyokwambia program ya kuutengeneza mfumo huu itakuwa ya wiki 4.

Wiki 3 za mwanzo tutaanza kwa kutengeneza kila kitu kinachohitajika kwenye hatua ya pili ya after click experience.

Maneno ambayo yataandikwa kwenye sales page yako kumshawishi mgonjwa kuwa tayari kutoa hela yanaandikwa kwa kutumia ujuzi wa Copywriting.

Kabla sijakwambia copywriting ni nini, nianze kwa kukwambia kwamba:

Copywriting sio AIDA.

Video nyingi za YouTube zinaongelea sana kuhusu AIDA matokeo yake mtu kujua AIDA ni nini anajiona anajua ujuzi huu wa Copywriting.

Mfumo wangu wa mwanzo ulifeli kwasababu kwa kujua AIDA nilijiona najua ujuzi huu wa Copywriting kumbe hata sijui. Nilijikuta naandika maelezo ya hovyo ambayo hata hayana ushawishi kwa mgonjwa kunipatia pesa pindi anapomaliza kuyasoma. Kwahiyo...

AIDA ni kama algebra kwenye hesabu. Unahisi kuijua topic ya algebra ndo kuijua hesabu?

Jibu ni hapana.

Kuna mengi sanaaaaa ambayo yamejificha nyuma ya pazia kuhusu ujuzi huu.

Kiufupi…

Copywriting ni ujuzi wa kuandika maandishi ambayo yanaiuza bidhaa yako kwa mteja kupitia yeye kuyasoma hayo maandishi pasipo wewe kuwepo wakati yeye anayasoma hayo maandishi.

Uandishi wa maneno haya haufuati taratibu za uandishi wa shuleni.

Kwanza ukiandika maneno haya ukampelekea mwalimu wako wa kiswahili atatapika kabisa maana kiswahili chako kitakuwa hakijanyoka wala kufuata tarataibu za uandishi wa shuleni.

Lakini chakushangaza maneno hayo hayo yataweza KUWASHAWISHI wagonjwa wakutumie hela kiurahisi bila hata kuongea nao au kuchat nao.

Kwahiyo hata kama ulifeli somo la kiswahili shuleni uandishi wa maneno haya hauna uhusiano kabisa na taratibu za uandishi wa shuleni.

Sasa... ujuzi huu wa copywriting au uandishi wa maneno ambayo yatauza bidhaa kwa niaba yako unafuata hatua 3 zifuatazo:

  • Hatua ya kwanza: Kufanya utafiti
  • Hatua ya pili: Kuandika maandishi au ujumbe wako kwa mara ya kwanza
  • Hatua ya tatu: Kufanya marekebisho na kukosoa makosa uliyoyafanya kwenye hatua ya pili.

Kwahiyo kwenye program yetu ya CAE ya wiki 4 tutakachokifanya kila wiki kwa mapana zaidi ni kama ifuatavyo:

Wiki ya kwanza: Kufanya Utafiti kwa kutumia akili ya bandia (ChatGPT)

Kama nilivyokwambia kwamba ujuzi huu wa copywriting una hatua tatu. Hatua ya kwanza ambayo ni kufanya utafiti.

Kwahiyo kwenye wiki ya kwanza ya program yetu tutatumia akili ya bandia kufanya utafiti ukamilike ndani ya masaa au siku kadhaa.

Tutafanya utafiti wa mambo 2.

Moja: kuhusu mteja wako na mbili: kuhusu bidhaa yako (zako).

Lengo la kutumia akili bandia kufanya utafiti kuhusu mteja wako ni kutaka kujua na kupata maneno ambayo ukiyatumia yatamshawishi mgonjwa akiyasoma awe tayari kutoa pesa kununua virutubisho lishe vyako.

Na lengo la kutumia akili ya bandia kufanya utafiti kuhusu bidhaa yako ni kutaka kujua ni maelezo gani yanayoihusu bidhaa yako ukimwambia mgonjwa atakuwa na shauku kubwa ya kutaka kuinunua bidhaa yako.

Kwahiyo mwisho wa wiki ya kwanza:

  • Utakuwa tayari umejua ni maneno gani kuhusu mteja wako (Mgonjwa) ukiyaandika yatamshawishi kutoa pesa kiurahisi kununua bidhaa yako

  • Utakuwa tayari umejua ni sehemu ipi ya bidhaa yako uielezee ambayo kwa 100% itamfanya msomaji (mgonjwa) kuwa na shauku kubwa sana ya kununua bidhaa yako
  • Utakuwa tayari una maelezo ambayo yatakutofautisha wewe na wachana wenzako hivyo kufanya wateja wakukimbilie na kukukumbuka wewe daima

  • Utakuwa tayari unajua maelezo ambayo hata siku moja hutakiwi kumwambia mgonjwa kama unataka anunue virutubisho lishe vyako (Hii ni muhimu sana maana karibia kila networker anafanya kosa hili ndio maana ni ngumu kuuza virutubisho lishe kwa wateja wapya kila mwezi)

  • Utakuwa tayari una taarifa ambazo ukiziandika zitamfanya msomaji akuamini na hivyo kuwa na shauku kubwa ya kununua bidhaa zako 

Baada ya hapo tunaendelea na…

Wiki ya pili: Kuandika maandishi au ujumbe wako kwa mara ya kwanza Na kufanya marekebisho sehemu ambayo utakuwa umekosea.


Wiki ya kwanza inaisha ukiwa unajua ni nini uandike na usiandike.

Kwahiyo wiki ya pili nakufundisha hatua 18 ambazo utazifuata wakati unaandika maelezo uliyoyapata kutoka kwenye utafiti uliofanya wiki ya kwanza kwa kutumia akili ya bandia.

Kwa kufuata hatua hizi 18 utawasilisha (Utaandika) kwa mara ya kwanza maelezo uliyoyapata kwenye utafiti wa wiki ya kwanza pasipo kujali makosa na mpangilio wa sentensi zako.

Si hivyo tu…

Nitakupatia sales page zangu 3 ambazo zishaniingizia faida ya zaidi ya 30,000,000/= ili uzitumie kama mfano wakati unaandika maelezo yako kwa mara ya kwanza.

Baada ya kukamilisha kuandika maandishi yako kwa mara ya kwanza kwa kufuata hatua 18 nitakazokufundisha na kuangalia jinsi nilivyoandika kwenye sales page zangu 3, inafuata hatua ya kukagua ulichokiandika na kufanya marekebisho ambayo nitakwambia uyafanye.

Mpaka wiki ya pili kuisha:

  •  Utakuwa tayari una ujumbe wa maandishi ambao mgonjwa akiusoma lazima atoe pesa anunue bidhaa yako.
  •  Utakuwa tayari umeandika ujumbe ambao utaitetea bei ya bidhaa yako hivyo kumfanya mgonjwa kuona bei si kitu ukilinganisha na faida za bidhaa yako (Hii itafanya iwe rahisi sana kuiuza bidhaa yako hata kama ni bei ghali)
  •  Utakuwa tayari umeandika ujumbe ambao unaielezea bidhaa yako kwa mapana hivyo kumfanya mgonjwa alidhike kwa maelezo yako na kuwa tayari kutoa pesa yake

Mwisho wa wiki ya pili habari ya ujuzi wa copywriting inakuwa imeishia hapo. Tunaendelea na…

Wiki ya tatu: Kutengeneza sales page.


Baada ya kuwa umekamilisha kuandika ujumbe wako kwenye wiki ya pili, wiki ya tatu tunatumia ujumbe huo kutengeneza ukurasa kama huu unaosoma muda huu.

Ukurasa huu unaitwa sales page.

Tunatengeneza ukurasa ambao utapatikana online masaa 24 hata kama ukiwa umelala au unafanya shughuli zako zingine ili wagonjwa muda wowote waweze kusoma ujumbe wako na kuwa tayari kununua bidhaa yako (zako)

Kutengeneza ukurasa kama huu sio kazi na wala sio lazima uwe na tovuti yako.

Hata kama huna tovuti yako nitakuelekeza jinsi ya kutengeneza ukurasa kama huu ambao utakuwa ni sales page maalumu kwa ajili ya kuiuza bidhaa yako masaa 24.

Baada ya kutengeneza sales page, tutatengeneza fomu ya mgonjwa kuweka ODA kisha link ya fomu hiyo tutaiweka kwenye sales page yako ili mgonjwa ambae yupo tayari kununua bidhaa yako abonyeze link ambayo itampeleka kwenye ukurasa wenye fomu ya kuweka ODA.

Nitakuelekeza jinsi ya kutengeneza fomu katika namna ambayo mgonjwa akiweka ODA wewe unatumiwa ujumbe kwenye email yako kukujulisha kuhusu ODA hiyo.

Mpaka wiki ya tatu kuisha:

  •  Utakuwa tayari una mfumo ambao unafanya kazi masaa 24 kukuuzia bidhaa zako
  •  Utakuwa tayari umetengeneza mfumo ambao utamfanya mgonjwa akupe umakini wake wote wa kusoma ujumbe wako tofauti na whatsapp. Hali hii itafanya mgonjwa aone thamani ya bidhaa yako kwake na hivyo kufanya iwe rahisi yeye kukupatia pesa licha ya gharama za dozi yako kuwa juu.
  •  Utakuwa tayari umetengeneza mfumo ambao utakupatia uhuru wa muda wa kufanya mambo yako mengine wakati mfumo ukifanya kazi ya kuiuza bidhaa yako.

  •  Utakuwa tayari umetengeneza mfumo ambao utaweza kumudu idadi yoyote ile ya wagonjwa hivyo kufanya iwe rahisi kutengeneza faida kubwa kila mwezi bila kikomo.
  •  Utakuwa tayari na mfumo ambao utakufanya useme kwaheri ya kuonana whatsapp, messenger au Instagram inbox na karibu mfumo wa kuuza bidhaa zako pasipo kuchat na mgonjwa yeyote.

Baada ya hapo tunamalizia…

Wiki ya nne: Kutangaza Facebook Na Instagram.

Baada ya utengenezaji wa sales page kukamilika ndani ya wiki ya tatu, sasa wiki ya nne tunaanza kurusha matangazo ya kulipia Facebook na Instagram.

Kuanzia wiki 1-3 hakuna hela yoyote itakayohitajika wakati unatengeneza mfumo wako.

Pesa itakuja kuhitajika hapa kwenye wiki ya nne ya kurusha matangazo ya kulipia Facebook na Instagram.

Hata hivyo…

Jinsi utakavyorusha matangazo yako ni tofauti kabisa.

Na utofauti unaanzia kwenye kutengeneza meta pixel.

Meta pixel ni maandishi fulani (Code) ambayo unayakopi kutoka kwenye business manager yako na kuyapesti kwenye sales page yako.

Kwahiyo nitakuelekeza jinsi ya kuyakopi na kuyapesti maneno hayo kwenye sales page yako. Ni rahisi sana kama kubonyeza on na off kwenye switch ya umeme.

Kazi ya hii meta pixel ni kutunza taarifa za kila atakaye tembelea sales page yako. Kwakua sales page yako itatembelewa na watu wenye uhitaji wa bidhaa zako maana yake hii pixel itakuwa inatuma taarifa Facebook au Instagram za aina ya watu ambao ni sahihi kuja kwenye sales page yako na hivyo kufanya sales page yako itembelewe na watu sahihi wenye uhitaji wa kununua bidhaa zako.

Baada ya hapo kitu kingine tutakachokifanya ni…

“Configuring the content view event” (Utanisamehe Kiswahili chake kimenishinda) lakini maana yake ni kwamba kuna seting za kawaida ambazo nitakuelekeza uzifanye ambazo zitalenga kutoa taarifa Facebook kwamba watu wanaotoka Facebook au Instagram kupitia matangazo ya kulipia wanasoma kweli ulichokiandika kwenye sales page yako.

Kwa kufanya hivyo utaweza kurusha matangazo ambayo dhumuni (objective) la tangazo lako litakuwa ni “sales” badala ya “Traffic”

Fb campaign objectives

Watu wamezoea wakirusha matangazo matokeo wanayapima kwa kuangalia idadi ya watu walioclick link kwenye tangazo (Link Clicks). Wasichojua ni kwamba idadi kubwa ya ambao wanaclick kwenye link hawafiki whatsapp. Ndio vile unashangaa walioclick ni mfano 200 lakini ambao wamefika whatsapp ni 20. Unajiuliza hao 180 wengine wameenda wapi.

Jibu ni kwamba wengine wanaishia juu kwa juu. Hawafiki na kibaya zaidi Facebook yeye anahesabu kama link click wawe wamefika au hawajafika shauri zako.

Lakini mimi naenda kukufundisha jinsi ya kurusha matangazo kwa kuangalia “content view” au “Landing page view” Maana yake ni kwamba itamlazimu Facebook ahakikishe mtu akibonyeza link, mtu huyo anafika kabisa kwenye sales page yako. Hii itafanya watu wote waliobonyeza kwenye link wafike kabisa sehemu uliyokusudia wafike. Na kwakua sales page yako itakuwa kama mdomo wa mamba mwenye njaa kali mtu akifika hachomoki.

Na Kwakuwa tushaseti meta pixel kwenye sales page yako, kwahiyo itakuwa ni rahisi Facebook kujua kama watu wanafika kweli maana pixel itakuwa inamjulisha kama wanafika kweli na kusoma ulichokiandika.

Kwahiyo mpaka wiki ya nne kuisha:

  • Utakuwa tayari unajua jinsi ya kurusha matangazo ambayo watu wakibonyeza kwenye link wanafika kabisa kwenye sales page yako. Hii itakufanya utengeneze faida kubwa kwasababu watu wengi wakitembelea sales page yako utaweza kupata watu wengi wa kuweka ODA.
  • Utakuwa tayari umetengeneza mfumo ambao unatuma taarifa Facebook za kila atakaye tembelea sales page yako. Kutumwa kwa taarifa Facebook kuna faida kubwa kwasababu kutamwambia Facebook aina ya watu ambao inatakiwa ndio wayaone matangazo yako kwa wingi hivyo matangazo yako kuwafikia watu sahihi na kufanya upate wateja wengi.

Baada ya wiki 4 kuisha hongera sana. Sasa utakuwa umefuzu kutengeneza mfumo wa kukufanyia kazi masaa 24.

Lakini…

Sitakudanganya na kukwambia kwamba kazi hii itakayofanyika ndani ya wiki hizi 4 ni nyepesi. 

Kazi hii ni ngumu, inachosha sana na sio kwa ajili ya watu lelemama au wapenda vitu mtelezo.

Ndio maana program hii ya CAE sio kwa ajili ya kila mtu.

Nahitaji watu wachache tu wakujiunga kwenye hii program ambao watakuwa sahihi.

Watu ambao hawatakuwa na visingizio au uvivu wa kufanya utekelezaji wa kila kitu ambacho nitakifundisha kuweza kubadili biashara zao na maisha yao kiujumla.

Na sio watu ambao wataleta sababu 200 kwanini hawawezi kuitumia program hii kama daraja la kuwafikisha wanakotaka kwenda.

Ukweli ni kwamba licha ya program hii kuwa bora bila wewe kufanya kazi (Namaanisha kazi kweli) mfumo huu wa kukufanyia kazi masaa 24 hutaweza kuutengeneza.

Kazi kubwa ipo kwenye kuutengeneza mfumo huu. Lakini baada ya kukamilisha kuutengeneza mfumo huu kinachobaki ni furaha, neema, ndelemo na vifijo.

Kwahiyo kama upo tayari kukomaa kupata maumivu ya wiki 4 kwa ajili ya kubadili maisha yako basi nikwambie kwamba wakati wako umefika maana program hii ya CAE ipo kwa ajili ya kukupa maumivu ya wiki 4 tu lakini baada ya hapo wewe mwenyewe utajishukuru kwa kujiumiza kwa wiki 4 kwa faida ya maisha yako yote.

Kwasababu baada ya wiki hizi 4 utakuwa na uwezo wa kuandaa mfumo wako wa kuuza bidhaa za tatizo lolote lile la kiafya.

Fikiria downlines wako wataneemeka kwa kiasi gani endapo utakuwa na uwezo wa kumuandalia kila downline wako mfumo wake wa kumletea wateja hata kama atakuwa yupo bize na shughuli zake zingine.

Fikiria utakuwa na nguvu kiasi gani ya kumshawishi mfanyakazi ambae muda wake ni finyu kujiunga kwenye biashara yako (japokuwa Program hii haihusu kuingiza watu kwenye fursa) lakini itakufanya uwe mtu ambae kila mtu atatamani mfanye kazi pamoja ili afaidike kupata mfumo wa kumsaidia kupata mauzo pasipo kupoteza muda kuchat na wagonjwa whatsapp.

Si hivyo tu…

Fikiria unaamka asubuhi huna hili wala lile kuwasha tu data kwenye simu yako unatumiwa ujumbe kwenye email yako kuwa wagonjwa 4 au 5 au 7 wameweka ODA ya kuchukua bidhaa zako. Ni furaha kiasi gani utakuwa nayo. 

Kazi yako kila siku itakuwa ni moja. Kupiga simu kwa wagonjwa walioweka ODA ya kuchukua bidhaa kuwasiliana nao wakati unawafanyia delivery ya ODA zao.

Kazi hiyo unaweza kuifanya kwa ndani ya dakika 30 au chini ya hapo. Kwahiyo ukiwa na mfumo huu masaa karibia 23 na dakika kadhaa utayatumia kulala na kufanya mambo yako mengine wakati mfumo wenyewe unaendelea kufanya kazi ya kuiuza bidhaa yako.

Kukwambia ukweli mfumo huu ndo umebadilisha maisha yangu. Kila kitu ninachokiuza kwa sasa nakiuza kwa kutumia mfumo huu.

Bila mfumo huu nina uhakika 100% nisingeweza hata siku moja kutengeneza faida ya 5,000,000/= ndani ya mwezi mmoja kwa kuchat na wagonjwa whatsapp.


Hawa hapa ni baadhi ya wanafunzi wangu ambao wameshahitimu mafunzo ya program hii. Huyu wa kwanza anaitwa Benjamin.

L-1
L-2
L-3

Mfumo wake tayari unafanya kazi masaa 24 anapiga hela mpaka mimi mwenyewe mwalimu naanza kumuogopa mwanafunzi wangu kwa maokoto anayopata

Ben Lak 7 Testimonial

Mwingine huyu hapa ambae kamaliza program hivi karibuni na MFUMO wake tulikua tunaufanyia majaribio.

Mgina testimonial

Mwingine tena huyu hapa kamaliza mafunzo ya wiki nne na sasa tupo kwenye majaribio ya mfumo wake

Shafii testimonial-1
Shafii testimonial-1
Shafii testimonial-1
Shafii testimonial-2

Mwingine baada ya kuhitimisha kutengeneza mfumo wake na kuanza kuona matunda ana yafuatayo ya kusema...

Mohamed testimonial-3

Bado anaendelea kutoa ushuhuda wa kila mwezi. Hii inaonesha MFUMO unamuingizia kipato endelevu

Mwingine baada ya kuhitimisha kutengeneza mfumo wake na kuanza kuona matunda ana yafuatayo ya kusema...

Program hii ya Customer Acquisition Engine (CAE) inaanza lini?

Mafunzo ya program nzima kuanzia wiki ya kwanza mpaka wiki ya 4 yameshaandaliwa tayari.

Kwahiyo program ishaanza tayari ni wewe kujiunga na kuanza mafunzo haraka iwezekanavyo.

Na mafunzo haya yanatolewa kwenye tovuti yangu (Online) na sio kwa kukutana ana kwa ana na kuanza kufundishana.

Utapata kujifunza ukiwa sehemu yoyote ile hapa Tanzania na kwa muda wako.

Mafunzo ni ya wiki 4 lakini kama una kichwa chepesi unaweza kujifunza kila kitu ndani ya wiki moja. Uzuri ukishalipia mafunzo yatakuwepo siku zote, kwahiyo hata kama uelewa wako ni wa taratibu utamaliza kwa mda wako. Au kama ukimaliza mafunzo na kuhitaji kujikumbushia, mafunzo yatakuwepo siku zote.

Inagharimu kiasi gani kujiunga Kwenye Program hii ya Customer Acquisition Engine (CAE)


Nimetafuta kila kona kwa hapa Tanzania kuona kama kuna mtu anafundisha kama ninachokifundisha kwenye madarasa yake, taarifa mbaya ni kwamba sijafanikiwa kuona sehemu hata moja.

Lengo la kutafuta madarasa yanayofundisha kama ninachokifundisha ni kutaka kujua gharama zao zipoje lakini kwa hapa Tanzania sijaona hata mtu mmoja ambae anafundisha kama ninachokifundisha kwenye program hii.

Ikanibidi niangalie program za Marekani ambazo zinafundisha kama ninachokifundisha. Nikagundua gharama ya program hizo ni kuanzia dola 997 mpaka dola 3000 (2,442,650/= mpaka 7,350,000/=)

Kwahiyo nikisema gharama ya kujiunga kwenye program yangu ni milioni mbili (2,000,000/=) itakuwa ni bei rafiki sana ukizingatia mimi ntakuwa nauza kwa bei ya chini kabisa ya program zote za marekani zinazofundisha kama ninachokifundisha.

Lakini naenda kukushangaza hutaamini.

Pesa utakayolipia kujiunga kwenye program hii haifiki hata nusu ya hiyo milioni mbili.

Utajiunga kwenye program hii kwa punguzo la 75%. Yaani badala ya kulipia 2,000,000/= utajiunga kwenye program hii kwa…

500,000/=

Sawa na 18,000/= kila siku kwa muda wa wiki 4 za program

Hata hivyo nakupatia punguzo la bei zaidi.

Program hii niliizindua kwa mara ya kwanza mwaka 2023, ambapo ada ya kujiunga ilikuwa 350,000/= na wanafunzi 73 walilipa na kupata mafunzo haya. Baada ya dirisha hilo kufungwa, sikuongeza wanafunzi wapya.

Baada ya muda, nilifungua tena usajili kwa gharama ya 160,000/=, ambapo wanafunzi 133 walijiunga. Kisha nikafunga tena kwa zaidi ya mwaka mmoja bila kupokea wanafunzi wapya.

Sasa, kuanzia leo tarehe 24/08/2025, nimeamua kufungua dirisha la usajili kwa mara ya mwisho. Dirisha hili litabaki wazi kwa muda mfupi pekee, kisha nitafunga tena rasmi.

Hivyo basi, katika kipindi hiki cha upokeaji wa wanafunzi wapya, ada ya kujiunga na program hii ni...

95,000/= 

Hujasoma vibaya. Program ambayo baadhi ya wanafunzi walilipia 350,000/= na wengine 160,000/= lakini wewe utalipia 95,000/= tu.

Kwanini natoa punguzo la bei kubwa hivi?

Kuna sababu mbili za msingi.

Sababu ya kwanza: Hii ndiyo mara yangu ya mwisho kupokea wanafunzi kwa program hii. Baada ya dirisha hili kufungwa, sitafungua tena usajili. Kwa kifupi, nina mpango wa kuifunga program hii kabisa kwa sababu nitakuwa na majukumu mengine yatakayohitaji muda na nguvu zangu nyingi, hivyo sitakuwa na nafasi ya kuwasaidia wanafunzi kwenye changamoto zao kama nilivyokuwa nafanya awali.

Dirisha hili litabaki wazi kwa muda mfupi tu (na muda huo haujulikani). Baada ya hapo litafungwa rasmi. Kwa hiyo, ili usikose nafasi ya kupata mafunzo haya ya kipekee, jiunge sasa kabla hujachelewa.

Sababu ya pili: Kwasababu kutoa punguzo la bei kunafanya watu wengi wajiunge kwenye program na kwakua lengo langu ni kusaidia NETWORKERS wengi (kwa mara ya mwisho) waweze kuwa na MFUMO wa kuuza VIRUTUBISHO LISHE masaa 24 ndio maana natoa punguzo la bei kubwa zaidi.

Hata hivyo, kama ukijiunga kwenye program hii nitakuzawadia na BONUS zifuatazo kwa BURE kabisa kama asante ya kujiunga kwenye program hii.

BONUS-1: Dakika 60.

DAKIKA 60 COVER

Kitabu hiki kinafichua hatua 9 za kutengeneza mashine ya kunasa downlines wapya kwa kufanya kazi dakika 60 tu kila siku.

Kitabu hiki kinauzwa 20,000/= lakini kama utajiunga kwenye program hii leo utakipata BURE kabisa.

Thamani ya BONUS hii ni 20,000/=

BONUS-2: Facebook & Instagram Mapene

Hii ni course iliyokamilika ambapo nafundisha mbinu ya "Targeting Hack" kufanya matangazo ya kulipia mtandaoni (Fb & Insta) yenye kuanza kuleta mafuliko ya wateja Ndani Ya Masaa 72 au chini ya Hapo!

Wakati nimeileta sokoni course hii kwa mara ya kwanza nilikuwa naiuza kwa 80,000/= na watu wengi tu walinunua. Badae nikaamua nipunguze mpaka 35,000/= ambayo ndo bei yake mpaka sasa.

Wanafunzi ambao washajiunga kwenye course hii mpaka sasa kama unavyoona kwenye picha hapo juu ni 558.

Ikiwa utajiunga kwenye program hii ya CAE leo nitakuzawadia course hii kwa BURE kabisa.

Thamani ya BONUS hii ni 35,000/=


Bonus zote 2 Thamani yake Kwa Ujumla Ni 55,000/=


Lakini BONUS hizi 2 utazipata kwa BURE kabisa endapo utajiunga leo kwenye program hii ya Customer Acquisition Engine.


Kwahiyo kwa ujumla, hii hapa orodha ya vitu Vyote utakavyovipata kama utalipia leo:

  • Program ya Customer Acquisition Engine – Thamani yake 2,000,000/=
  • Kitabu cha Dakika 60 – Thamani yake 20,000/=
  • Course ya Facebook & Instagram Mapene – Thamani yake ni 35,000/=

Jumla ya Thamani ya Kila kitu utakachojifunza ni 2,055,000/= lakini wewe utalipia 95,000 Tu Kwa Leo kupata kila kitu.


Kwahiyo kwa 95,000/= utapata kugundua siri zote nilizozifundisha kwenye program hii.

Guarantee image

Kama baada ya wiki 4 utakuwa hujalidhishwa na mafunzo ya program hii (Kwa Sababu yoyote) nijulishe kupitia namba ya simu ambayo itakuwepo kwenye risiti ya malipo nitakurudishia pesa zako zote bila kinyongo chochote.

Hata hivyo nina uhakika utaipenda sana program hii na utalidhika kwa mafunzo nitakayokupatia.

Kwanza nadhani wewe mwenyewe utashangazwa kwa kile ambacho naenda kukufundisha kwenye program hii.

Ukweli ni kwamba, unaenda kuwa mtu wa tofauti kwa kuwa na mfumo ambao utakuwezesha kufanya kazi dakika 30 tu kila siku huku ukipata wateja wa kukupatia faida ya malengo yako ya kila mwezi.

UNACHOTAKIWA KUFANYA SASA HIVI NI HIKI:

Bonyeza hapa chini sehemu iliyoandikwa "LIPIA SASA" kufanya malipo ili uanze mafunzo haraka iwezekanavyo.

95,000/= | 2,000,000/= | Save 96%

Ahsante kwa kuchukua muda wako na kusoma maelezo haya. Ni matumaini yangu kwamba tutakutana kwenye program hivi karibuni.

Cheers,

Mr Bokko.

Copyright - Online Marketing System Pro

This site is not a part of the FacebookTM website or FacebookTM  Inc. Additinally, this site is NOT endorsed by FacebookTM  in any way. FACEBOOKTM is a trademark of FACEBOOKTM, inc.                

>
error: Copying is not allowed on this website
Powered by ProofFactor - Social Proof Notifications